Monday, July 24, 2017

NAIBU WAZIRI TAMISEMI SELEMANI JAFFO AKABIDHI HUNDI YA MILIONI 70 KWA VIJANA NA WANAWAKE, AIPONGEZA MANISPAA YA DODOMA , ATAKA HALMASHAURI ZINGINE KUIGA MFANO



Naibu waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI Selemani Jaffo akizungumza kabla ya kukabidhi mfani wa Hundi ya shilingi milioni 70 kwa wawakilishi wa vikundi vya wanawake na vijana  wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya fedha hizo zilizotolewa na Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma kwa ajili ya vikundi hivyo leo katika ukumbi wa Manispaa hiyo Wa pili kulia ni Meya wa Manispaa hiyo Mstahiki Profesa Davis Mwamfupe na kushoto ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi. PICHA NA RAMADHANI JUMA, OFISI YA MKURUGENZI.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi (kushoto) akitoa taarifa ya utangulizi kabla Naibu waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI Selemani Jaffo (wa pili kushoto) hajakabidhi mfano wa Hundi ya shilingi milioni 70 kwa wawakilishi wa vikundi vya wanawake na vijana  wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya fedha hizo zilizotolewa na Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma kwa ajili ya vikundi hivyo leo katika ukumbi wa Manispaa hiyo. Wa pili kulia ni Meya wa Manispaa hiyo Mstahiki Profesa Davis Mwamfupe. PICHA NA RAMADHANI JUMA, OFISI YA MKURUGENZI.


Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI Selemani Jaffo akikabidhi mfani wa Hundi ya shilingi milioni 70 kwa wawakilishi wa vikundi vya wanawake na vijana (kulia na kushoto) wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya fedha hizo zilizotolewa na Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma kwa ajili ya vikundi hivyo leo katika ukumbi wa Manispaa hiyo. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi.  PICHA NA RAMADHANI JUMA, OFISI YA MKURUGENZI.



................................................................


NAIBU Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI Selemani Jaffo ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma kwa kutekeleza Sera na maelekezo ya Serikali kwa vitendo ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa, asilimia 10 ya  fedha zinazotokana na mapato ya ndani zinatengwa na kutumika kwa ajili ya kuwawezesha Wanawake na Vijana.

Naibu Waziri Jaffo ametoa pongezi hizo wakati akikabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni 70 zilizotolewa na Manispaa hiyo kwa ajili vikundi vya Vijana na Wanawake katika hafla fupi ya makabidhianao iliyofanyika leo katika ukumbi wa Manispaa ya Dodoma.

Alisema Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma imeonesha mfano kwa vitendo na kwamba Halmashauri zingine zijifunze na kuiga, ambapo amedai hayo ni matokeo ya ushirikiano mzuri wa kazi uliopo kati ya Madiwani, Mkurugenzi, Wakuu wa Idara na Watumishi wote.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi  alisema fedha hizo zinatarajiwa kuvinufaisha vikundi 66, vikiwemo 18 vya vijana na 48 vya wanawake.

Alisema, Halmashauri hiyo imekuwa akitumia fedha za Mapato ya ndani kwa kuzingatia maelekezo ya Serikali ambapo pamoja na kutoa asilimia 10 kwa ajili ya vijana na wanawake, pia asilimia 30 inaelekezwa katika katika miradi ya Maendeleo ambapo mpaka sasa Kata 25 zimepatiwa sehemu ya fedha kwa ajili miradi ya maendeleo.

Aidha, Kunambi alisema kwa sasa Halmashauri hiyo inaanza kusajili vikundi vya walemavu ambavyo kwa mujibu wa Sera na Maelekezo ya Serikali vinatakiwa kupatiwa asilimia mbili ya Makusanyo ya fedha zinatokana na vyanzo vya ndani.

No comments:

Post a Comment