Ofisa mifugo wa Kata ya Chahanga katika Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma William Gervas akimpiga chapa Ng'ombe wakati wa zoezi la upigaji chapa mifugo linaloendelea katika Halmashauri hiyo.
|
Tuesday, November 28, 2017
UPIGAJI CHAPA MIFUGO WAENDELEA KUSHIKA KASI MANISPAA YA DODOMA
Monday, November 27, 2017
RC MAHENGE ATAKA MAMBO MATANO KUIPAISHA DODOMA
.......................................
MKUU wa Mkoa wa Dodoma
Dokta Binilith Mahenge amewataka watumishi na viongozi wa Halmashauri Mkoani humo
kuhakikisha wanayapa kipaumbele mambo
matano ikiwemo kudumisha hali ya Ulinzi na Usalama ambayo ndiyo nguzo muhimu inayopelekea shughuli nyingine za maendeleo
kufanyika kwa ufanisi ili kuifanya Dodoma ikue kwa kasi.
Mambo mengine aliyoyayaorodhesha
Mkuu huyo wa Mkoa kama dira ya kuharakisha maendeleo ni pamoja na utayari wa
kubadilika kwa watumishi na kutofanya kazi kwa mazoea, utoaji wa huduma bora na
zenye viwango kwa wananchi, kudumisha dhana ya Ushirikishwaji baina ya Taasisi
na miongoni mwa watumishi, na kuepuka migogoro baina ya watumishi ndani ya
Taasisi hali inayoweza kudumaza malengo ya Serikali katika kuwadumia wananchi.
Mkuu wa Mkoa Mahenge
aliyasema hayo wakati alipokuwa akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya
Manispaa ya Dodoma alipofanya ziara ya kujitambulisha katika Wilaya ya Dodoma
Novemba 24 mwaka huu.
Awali alipokea taarifa ya
maendeleo ya Wilaya iliyowasilishwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya
Dodoma Godwin Kunambi kwa niaba ya Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Dodoma ambaye pia ni
Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Vumilia Nyamoga.
MACHINGA MANISPAA YA DODOMA KUKABIDHIWA ENEO RASMI HIVI KARIBUNI, BIBI KIZEE AISHUKURU MANISPAA
..........................................
WAFANYABIASHARA wadogo
maarufu kama Machinga katika Manispaa ya Dodoma wanatarajiwa kupewa eneo
lililotengwa rasmi na Halmashauri ya
Manispaa hiyo kwa ajili ya biashara zao lililopo katika Kata ya Makole mjini
humo.
Halmashauri ya Manispaa ya
Dodoma chini ya Mkurugenzi Godwin Kunambi imekamilisha uwekaji wa miundombinu
muhimu katika eneo hilo maarufu kama ‘Makole D-Center’ ikiwemo choo, ambapo
wakati wowote wafanyabiashara hao watahamishiwa kwa utaratibu utakaoratibiwa na
Manispaa kwa kushirikiana na uongozi wa wafanyabiashara hao.
Katika hatua za awali za
maandalizi ya eneo hilo, Halmashauri
pamoja na mambo mengine, iliondoa makazi ya Bibi Elizabeth Sonyo aliyekuwa
akiishi katika eneo hilo kinyume cha Sheria.
Hata hivyo, kutokana na
Bibi huyo anayekadiriwa kuwa na umri wa zaidi ya miaka 75 kutokuwa na uwezo wa
kujenga, Manispaa ilibeba jukumu la kumjengea makazi mapya na bora zaidi katika
eneo jingine, ambapo amemshukuru Mkurugenzi wa Manispaa kwa kitendo hicho kwani
hakuwa na uhalali wa kisheria wa kuishi katika hilo na kwamba angeweza
kuondolewa bila kupewa msaada wowote.
Kwa mujibu wa Kaimu
Mhandisi wa Ujenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Ludigija Ndwata, kazi
iliyobaki ni kuweka mawe maalum (gravels) katika eneo hilo ili livutie zaidi na
liwe rafiki kwa wafanyabiashara na wateja, kabla ya matumizi kuanza.
Halmashauri ya Manispaa pia
inaandaa eneo la ‘Chaduru D-center’ kwa ajili ya kulirasimisha kwa matumizi ya wafanyabiashara
wadogo hususan akina mama wanaouza vyakula, mbogamboga, na matunda.
Thursday, November 16, 2017
WAKAZI 8570 MKONZE MANISPAA YA DODOMA WAPATIWA HUDUMA YA MAJI SAFI YA BOMBA
...............................................
WANANCHI 8570 wakazi wa
Kata ya Mkonze katika Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma wananufaika na huduma
ya maji safi ya bomba kufuatia kukamilika kwa mradi wa Maji katika Kata hiyo
ulitekelezwa na Manispaa hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa ya Mkurugenzi
wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi iliyowasilishwa kweye
Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), mradi huo uliotekelezwa
chini ya Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji awamu ya kwanza, ulianza
kujengwa Septemba, 2012 na kukamilika Machi, 2014 kwa gharama ya Shilingi 497,263,970
ukiwa na vituo 15 vya kutolea maji.
Kamati ya Bunge ya Hesabu
za Serikali za Mitaa (LAAC) ilitembelea mradi huo jana na kuishauri Halmashauri
ya Manispaa ya Dodoma kuharakisha taratibu za kukabidhi mradi huo kwa Mamlaka
ya Maji Safi na Maji Taka Dodoma (DUWASA) ambayo kwa mujibu wa sheria ndiyo
yenye dhamana ya kutoa huduma ya Maji mjini.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mheshimiwa
Vedasto Ngombale aliwaogoza wajumbe wa
Kamati yake katika ziara ya kukagua ufanisi wa mradi huo.
Akizungumza kwa niaba ya
Kamati katika eneo la mradi, Mheshimiwa Ngombale ambaye pia ni Mbunge wa jimbo
la Kilwa Kaskazini, alisema ni muhimu mradi huo kuwa chini ya DUWASA kwani
umeshakamilika na uko eneo la mjini, badala ya kuwa chini ya Manispaa na
kusimamiwa na Jumuiya ya Watumiaji Maji.
Kwa upande wake, Mkurugenzi
wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi aliahidi kutekeleza ushauri
na maelekezo yote ya Kamati hiyo kwa wakati ili malengo ya Serikali ya kusogeza
huduma muhimu karibu na wananchi yakamilike.
Tayari Halmashauri ya
Manispaa ya Dodoma iko katika hatua za mwisho za kukakabidhi mradi mwingine wa maji
kwa DUWASA uliotekelezwa katika Kata ya Ng’hong’ona ukiwa katika hatua ya
mwisho ya ukamilishwaji ambapo wananchi 8318 watanufaika na mradi huo wenye
vituo 20 vya kutolea maji.
Thursday, November 2, 2017
HALMASHAURI ZA DODOMA ZAPEANA SOMO, SHUGHULI YAANZIA MANISPAA YA DODOMA
Sehemu ya Wajumbe wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma wakifuatilia mkutano wa Baraza jana katika ukumbi wa Manispaa. |
Baadhi ya Wageni Waalikwa wakifuatilia Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Dodoma Robert Mwinje, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa ambaye pia ni Mwenyekiti wa ALAT Mkoa wa Dodoma White Zuberi (wa pili kushoto), na Mwneyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi Danford Chisomi (wa pili kulia). Kushoto ni Meya wa Jiji la Mbeya Mstahiki David Mwasilindi.
|
..................................................
HALMASHAURI zote nane za
Mkoa wa Dodoma zimekubaliana kuwa na utaratibu wa ziara za kubadilishana uzoefu
hususan katika uendeshaji wa vikao na mikutano ikiwemo Baraza la Madiwani.
Hayo yalisemwa jana na Meya
wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Mstahiki Profesa Davis Mwamfupe wakati
akiwatambulisha baadhi ya Wenyeviti na Wataalam wa Halmashauri za Wilaya za
Mkoani humo waliohudhuria mkutano wa Baraza la Madiwani wa Manispaa ya Dodoma
ikiwa ni mwanzo wa utekelezaji wa ushirikiano huo.
Mkutano huo uliofanyika
katika ukumbi wa Manispaa ya Dodoma, ulihudhuriwa na Mwenyekiti wa Halmashauri
ya Wilaya ya Kongwa Mheshimiwa White Zuberi Mwanzalila ambaye pia ndiye
Mwenyekiti wa ALAT Mkoa wa Dodoma, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi Mheshimiwa
Danford Chisomi, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino Mheshimiwa Samweli
Kaweya na Mkurugenzi wa Halmashauri ya
Wilaya ya Bahi Rachel Chuwa.
Halmashauri zinazounda Mkoa
wa Dodoma ni Manispaa ya Dodoma, Bahi, Chamwino, Kongwa, Mpwapwa, Kondoa Mji,
Kondoa Vijijini, na Chemba.
Subscribe to:
Posts (Atom)