Friday, April 7, 2017

BANKI YA DUNIA YAKAGUA MIRADI MANISPAA YA DODOMA




 Mhandisi wa Mazingira Manispaa ya Dodoma Barnabas Faida (katikati) akifafanua jambo wakati wa ziara ya ukaguzi wa Dampo la kisasa la kuhifadhi taka ngumu iliyofanywa na maafisa kutoka  Benki ya Dunia jana Aprili 6, 2017.


Mwakilishi kutoka Benki ya Dunia  (katikati) akishudia kazi ya kumwaga na kuhifadhi taka ngumu katika Dampo la kisasa lililopo Chidaya Manispaa ya Dodoma wakati yeye na ujumbe wake walipofanya ziara ya kukagua miradi inayofadhiliwa na Benki hiyo jana April 6.  Wa pili Kulia  (mwenye suti) ni Mhandisi wa Ujenzi wa Manispaa ya Dodoma Lusako Kilembe na wa pili kushoto ni Mhandisi wa Mazingira Manispaa ya Dodoma Barnabas Faida. 

Kazi ya umwagaji na uhifadhi wa taka ngumu ikiendelea katika Dampo la Chidaya


Kazi ya umwagaji na uhifadhi wa taka ngumu ikiendelea katika Dampo la Chidaya.


Barabara ya 'Independence Square' ni miongoni miradi ya barabara za mji wa Dodoma iliyojengwa kwa kiwango cha lami kwa ufadhili wa Benki ya Dunia


TIMU ya maafisa kutoka Benki ya Dunia wamefanya ziara ya kukagua mradi  wa dampo la kisasa na Barabara zinazofadhiliwa na Benki hiyo katika Manispaa ya Dodoma chini ya Mradi wa Uimarishaji wa Miji Tanzania (TSCP).

Ziara hiyo ilifanyika jana April 6, 2017 ambapo timu hiyo ilitembelea eneo la Chidaya unakotekelezwa mradi wa dampo la kisasa linalotumia teknolojia ya kuzika taka (Land Fill) na kufurahishwa na maendeleo ya mradi ambao umeashaanza kufanya kazi huku ujenzi ukiwa katika hatua za mwisho.

Aidha ujumbe huo ulitembelea barabara zilizojengwa chini ya mradi huo unaotekelezwa katika Manispaa Saba Tanzania Bara pamoja na Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA).



Awali ujumbe huo ulikutana na Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi na kufanya nae mazungumzo mafupi, ambapo aliishukuru Benki ya Dunia kwa kusaidia kuboresha miundombinu katika Manispaa ya Dodoma huku akiiomba kuendelea kutoa ufadhili zaidi ili kuufanya mji wa Dodoma kuwa wa kisasa zaidi hivyo kuendana na hadhi yake ya kuwa makao makuu ya Nchi.



No comments:

Post a Comment