Friday, April 28, 2017

HALMASHAURI ZAKARIBISHWA KUWEKEZA DODOMA




Meya wa Manispaa ya Kigamboni Mstahiki Maabad Hoja (wa pili kulia) na baadhi ya Madiwani na Wataalam wa Manispaa hiyo wakiwa katika ziara ya Mafunzo katika Dampo la Kisasa linalotumia  teknolojia  ya kuzika taka ngumu (Landa Fill) katika  Manispaa ya Dodoma jana Aprili 27, 2017. Wa kwanza kulia ni Naibu Meya wa Manispaa ya Dodoma Jumanne Ngede.
Meneja wa Dampo la Kisasa linalotumia  teknolojia  ya kuzika taka ngumu (Landa Fill) katika  Manispaa ya Dodoma John Chiwanga ( kushoto ) akitoa maelezo kwa Meya wa Manispaa ya Kigamboni Mstahiki Maabad Hoja (wa pili kulia) na baadhi ya Madiwani na Wataalam wa Manispaa hiyo walipokuwa katika ziara ya Mafunzo  jana Aprili 27, 2017. Wa kwanza kulia ni Naibu Meya wa Manispaa ya Dodoma Jumanne Ngede.

Mkuu wa Idara ya Usafi na Takangumu  Dickson Kimaro (aliyesimama) akitoa taarifa ya hali ya Usafi katika Manispaa ya Dodoma kwa Meya wa Manispaa ya Kigamboni Mstahiki Maabad Hoja (hayupo pichani) na baadhi ya Madiwani na Wataalam wa Manispaa hiyo walipokuwa katika ziara ya Mafunzo  jana Aprili 27, 2017. Waliokaa ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Kigamboni Rahel Muhando na Naibu Meya wa Manispaa hiyo Amini Sambo.

Mhandisi wa Mazingira wa Manispaa ya Dodoma Barnabas Faida (kulia) akitoa maelekezo kwa  Meya wa Manispaa ya Kigamboni Mstahiki Maabad Hoja (katikati) na baadhi ya Madiwani na Wataalam wa Manispaa hiyo walipokuwa katika ziara ya Mafunzo  jana Aprili 27, 2017, ya jinsi mashine za kupimia uzito wa taka ngunu inavyofanya kazi katika mzani uliopo kwenye Dampo la Kisasa linalotumia  teknolojia  ya kuzika taka ngumu (Landa Fill) katika  Manispaa ya Dodoma. PICHA ZOTE: RAMADHANI JUMA-OFISI YA MKURUGENZI 


MKURUGENZI wa  Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi ametoa wito kwa Halmshauri nchini kuwekeza katika Manispaa ya Dodoma kama njia mojawapo ya kujiongezea mapato ya ndani.

Ametoa wito huo jana wakati wa kikao cha majumuisho ya ziara ya mafunzo ya Madiwani na Wataalam wa Manispaa ya Kigamboni Mkoa wa Dar es Salaam waliyoifanya katika Manispaa ya Dodoma.

Kunambi aliwaeleza wageni  hao kuwa, Manispaa ya Dodoma ina fursa nyingi za uwekezaji ikiwa ni pamoja na ujenzi wa hoteli za kisasa, majengo ya Ofisi, na miundombinu mingine ikizingatiwa kuwa kuna rasilimali ardhi ya kutosha na sasa ni Makao Makuu ya Nchi.

Msafara wa watu 20 wakiwemo Madiwani na Wataalam kutoka Manispaa ya Kigamboni  ukiongozwa na Meya wa Manispaa hiyo Mstahiki  Maabad Hoja  walifanya ziara ya mafunzo juu ya usafi wa Mazingira na uhifadhi wa taka kwa kutumia teknolojia ya kisasa ya kuzika taka ardhini (Land Filling) ambapo Manispaa ya Dodoma inafanya vizuri kupitia Dampo lililopo katika Kata ya Ntyuka katika Manispaa hiyo.


Pia ziara yao ililenga kulijifunza kuhusu suala la utozaji na ukusanyaji wa kodi mbalimbali unaofanywa na Manispaa.

No comments:

Post a Comment