Thursday, May 25, 2017

MADIWANI MANISPAA YA DODOMA WAMPA KONGOLE RAIS MAGUFULI



Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Christina Mndeme (kulia) akiongoza wimbo maalum wa kumsifu na kumpongeza Mheshimiwa Rais wa Jamahuri ya Muungano wa Tanzania Dokta John Magufuli kwa uamuzi wake wa kuifuta Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) Katikati ni Naibu Meya  wa Manispaa Dodoma Jumanne Ngede na kushoto ni Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Godwin Kunambi


Waheshimiwa Madiwani ambao ni wajumbe wa Baraza la Madiwani la Manispaa ya Dodoma  wakiimba wimbo maalum wa kumsifu na kumpongeza Mheshimiwa Rais wa Jamahuri ya Muungano wa Tanzania Dokta John Magufuli kwa uamuzi wake wa kuifuta Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) Wimbo huo ulikuwa ukiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Christina Mndeme (Hayupo pichani).



BARAZA la Madiwani wa Manispaa ya Dodoma limempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dokta John Magufuli kwa hatua  yake ya kuivunja rasmi iliyokuwa Mamlaka ya Ustawishaji Makao  Dodoma (CDA) na kwamba hatua ni maamuzi muhimu na sahihi kwa maendeleo  ya Manispaa na Mkoa wa Dodoma kwa ujumla.

Wajumbe wa Baraza hilo likiongozwa na Mwenyekiti wake ambaye ni Naibu Meya  wa Manispaa hiyo Jumanne Ngede walikutana jana kwenye ukumbi wa Manispaa kwa ajili ya  Mkutano Maalum wa kuzungumza na vyombo vya Habari na kutoa  tamko rasmi la kumpongeza Rais Magufuli kwa hatua hiyo.

Walidai hatua hiyo itafungua milango kwa wawekezaji  wengi  kuwekea Dodoma kutokana  na taratibu za kupataji na umiliki wa ardhi kuboreshwa chini ya Manispaa, ikiwemo utolewaji wa hati za umiliki wa ardhi za miaka 99 badala zile za miaka 33 zilizokuwa zikitolewa na iliyokuwa CDA.


Mei 15 mwaka huu,  Mheshimiwa Rais Dokta John Magufuli alisaini tamko la Amri ya Rais la kuivunja iliyokuwa CDA baada ya kujiridhisha kuwa kwa sasa hakuna mahitaji ya kuwa na mamlaka hiyo iliyoanzishwa kwa Amri ya Rais mwaka 1973, na kwamba shughuli, mali, na watumishi 284 wanakuwa chini ya Manispaa ya Dodoma.

No comments:

Post a Comment