Tuesday, October 24, 2017

WAKUU WA IDARA MANISPAA YA DODOMA WAINGIA MTAANI KUSAKA KODI

Kiongozi wa kikosi kazi cha Wakuu wa Idara Dickson Kimaro (wa pili kushoto ) akimuhoji mmoja wa Wafanyabiashara wa Eneo la 'Mambo Poa' wakati wa zoezi la uhakiki wa nyaraka mbalimbali za biashara.

Mmoja wa wafayabiashara ya chakula maarufu Mama Lishe (kulia) akilipa kodi kwa Maafisa wa Manispaa ya Dodoma wakati wa zoezi la kuhakiki nyaraka za kisheria za kuendesha biashara.


Mhasibu wa Mapato wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Mganula Mbogoni akiweka utepe ikiwa ni ishara ya kulifunga moja ya duka ambalo mmiliki wake hakukidhi masharti ya kisheria ya kufanya biashara ikiwas ni pamoja na kutokuwa na Mkataba hai wa Pango na Leseni ya Biashara.

............................................

MENEJIMENTI ya Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma imeanza zoezi la uhakiki wa nyaraka mbalimbali kwa wafanyabiashara waliopanga vibanda vya biashara vinavyomilikiwa na Manispaa hiyo, ambapo wakuu wa Idara wanatekeleza zoezi hilo kwa kupita katika vibanda vyote vilivyopangishwa kwa wafanyabiashara.

Nyaraka zinazohakikiwa ni mikataba ya upangishaji wa chumba cha biashara na leseni za biashara husika, ambapo maeneo mengine kama viwanda vya matofali, maeneo ya kuoshea magari, na maeneo ya kuchomelea vyuma pia yatahusishwa katika uhakiki huo ili kujiridhisha endapo biashara hizo zinaendeshwa kwa kuzingatia sheria na taratibu kama inavyopaswa.


Zoezi hilo la siku tatu limeanza vizuri ambapo baadhi ya Wafanyabiashara ambao mikataba yao ya upangishaji ilimalizika wameonesha ushirikiano kwa kulipia huku wengine wakifungiwa maduka kwa kushindwa kufanya hivo.


No comments:

Post a Comment