Friday, October 27, 2017

WANANCHI MANISPAA YA DODOMA WATAKIWA KUHUDHURIA MIKUTANO YA MANISPAA

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi (kushoto) akizungumza wakati wa Mkutano wa awali wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo Oktoba 25 mwaka huu. Katika ni Naibu Meya wa Manispaa hiyo Jumanne Ngede na kulia ni Afisa wa Serikali za Mitaa Kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Emmanuel Kuboja.   (PICHA-OFISI YA MKURUGENZI)

..............................................

WAKAZI wa Manispaa ya Dodoma wameshauriwa kuhudhuria mikutano ya Baraza la Madiwani ili kupata taarifa za miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na Manispaa yao na kujua kazi inayofanywa na Madiwani waliowachagua.

Wito huo umetolewa na Naibu Meya wa Manispaa ya Dodoma Jumanne Ngede kuelekea Mkutano wa Baraza hilo wa kisheria kwa robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2017/18  utakaopokea taarifa mbalimbali za Manispaa hiyo kitakachonyika Oktoba 31 mwaka huu katika ukumbi wa Manispaa.

Naibu Meya Ngede alitoa wito huo wakati alipoongoza Mkutano wa awali wa Baraza la Madiwani la Manispaa hiyo lililopokea taarifa za utekelezaji wa miradi kutoka katika Kata zote 41 za Manispaa ya Dodoma Oktoba 25 mwaka huu.

Aliiagiza Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma kuongeza matangazo kwa wananchi kuhusu tarehe ya Mkutano huo ili waweze kuhudhuria kutokana na umuhimu wa mkutano huo ambao ni wa wazi.

No comments:

Post a Comment