Wednesday, July 20, 2016

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA KUWEKA JIWE LA MSINGI UKARABATI WA UWANJA WA NDEGE WA DODOMA


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANI

                                                  WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO                                                     
MAMLAKA YA VIWANJA VYA NDEGE
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim M. Majaliwa kesho, tarehe 20/07/2016, anatarajiwa kuweka jiwe la msingi la mradi wa ukarabati na upanuzi wa Kiwanja cha ndege cha Dodoma.
Ukarabati huo utajumuisha urefushaji wa barabara ya kuruka na kutua ndege hadi kufikia urefu wa kilometa 2.5 kutoka Kilometa 2 za awali.
Kurefushwa kwa barabara hiyo, sasa kutatoa fursa kwa ndege kubwa Bombardier Q400, Gulfstream 550, ATR 72 n.k zenye uwezo wa kubeba abiria 90.
Ukarabati huo unafanyika kwa fedha za Serikali ya Tanzania na unasimamiwa na Wahandisi wa Mamlaka ya Viwanja Vya Ndege Nchini kwa ushirikiano  na Wakala wa Barabara nchini (TANROADS).
Ukarabati na upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Dodoma ni miongoni  mwa Miradi mbali mbali inayotekelezwa na Mamlaka ya viwanja Vya Ndege nchini kama vile Viwanja vya Tabora, Bukoba, Kigoma na Mwanza ambayo imekwisha anza na miradi mipya ya viwanja vya ndege vya Shinyanga na Sumbawanga itakayoanza hivi karibuni.
Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) ni wakala wa viwanja vya ndege iliyoanzishwa kwa Tangazo la Serikali Namba 404 la mwaka 1999, chini ya Sheria ya Wakala za Serikali Na. 30 ya mwaka 1997.
Dira:           Kuwa mtoaji wa Huduma za Viwanja vya Ndege kwa kiwango cha Kimataifa
                        Dhima:         Kutoa Huduma Bora na Viwezeshi katika Viwanja vya Ndege kwa kuzingatia ufanisi katika matumizi ya rasilimali zilizopo
Imani kuu za Mamlaka:
Kuwajali Wateja
Kuwaendeleza Wafanyakazi wa Mamlaka
Ulinzi na Usalama Viwanjani
Kufanya kazi kwa pamoja
Kuwa na Uongozi wa Mabadiliko
Uadilifu
IMETOLEWA NA KITENGO CHA SHERIA NA MAHUSIANO TAA
CHANZO: FULLSHANGWE BLOG

No comments:

Post a Comment