Tuesday, July 26, 2016

VIKUNDI VYA USHIRIKA NA WAJASIRIAMALI DODOMA WATAKIWA KUJITANUA KIMIRADI


VIKUNDI mbalimbali vya wanaushirika na wajasiriamali katika Manispaa ya Dodoma wameshauriwa kuweka mipango ya kuongeza miradi zaidi ili kukuza mitaji yao na kufikia malengo ya kuundwa kwa vikundi hivyo.

Ushauri huo umetolewa na Naibu Meya wa Manispaa ya Dodoma Jamanne Ngede wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi iliyofanywa na wajumbe wa Kamati ya Fedha na Utawala katika Kata mbalimbali za Manispaa hiyo.
Aliwataka wanaushirika na vikundi vingine vya wajasiriamali kuunda vikundi vidogo miongoni mwao na kupeana mitaji ili kukuza wigo wa kazi zao na hivyo kujiongezea kipato zaidi.
Miongoni mwa vikundi vilivyokaguliwa na Kamati hiyo ni kikundi cha Kasi Mpya kilichopo katika Kata ya Msalato ambacho ni cha akina mama wanaojishughulisha na ufugaji wa kuku wa mayai na utengenezaji wa batiki.
Kikundi hicho chenye wanachama kumi kina kuku 300 wa mayai ambapo kwa siku moja hukusanya kati ya trei sita hadi kumi za mayai, huku trei moja ya mayai ikiwa na thamani ya shilingi 8,500.
Katika kukiongezea nguvu kikundi hicho cha akina mama, Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma imekipatia mkopo wa shilingi 806,450 kwa ajili ya kununua chakula cha kuku na madawa ambapo tayari kimeanza kufanya marejesho ya mkopo huo kwa kutoa shilingi 148,000.

 Naibu Meya wa Manispaa ya Dodoma Jamanne Ngede (mwenye kaunda suti) na ujumbe wake wakitazama kuku waliopo katika moja ya mabanda ya wajasiriamali wa kikundi cha akina mama cha Kasi Mpya kilichopo katika Kata ya Msalato katika Manispaa hiyo. Akina mama hao wanafuga kuku wa mayai wapatao 300.


  Baadhi ya kuku wanaofugwa na akina mama hao

 Kati ya trei 6 hadi 10 za mayai huokotwa kwa siku


 Baadhi ya akina mama ambao ni wanachama wa kikundi hicho


 Naibu Meya wa Manispaa ya Dodoma Jamanne Ngede (kulia) akipokea zawadi ya mayai kwa niaba ya Kamati ya Fedha na Utawala kutoka kwa wajasiriamali hao.

 Naibu Meya wa Manispaa ya Dodoma Jamanne Ngede (kulia) akivishwa zawadi ya batiki aliyopewa na wajasiriamali wa kikundi cha akina mama cha Kasi Mpya kilichopo katika Kata ya Msalato katika Manispaa hiyo. 


Naibu Meya wa Manispaa ya Dodoma Jamanne Ngede (aliyejifunika batiki katikati waliokaa) na wajumbe wengine wa Kamati ya Fedha na Utawala wa Manispaa ya Dodoma John Matonya (kushoto) na Jamal Ngalya (wa pili kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na kikundi wajasiriamali cha akina mama cha Kasi Mpya kilichopo katika Kata ya Msalato katika Manispaa hiyo, na baadhi ya wataalam wa Manispaa hiyo. 

No comments:

Post a Comment