Thursday, June 8, 2017

'KITIMOTO' MARUFUKU MAKAO MAKUU DODOMA

DAKTARI wa Mifugo Wilaya ya Dodoma Mjini Innocent Kimweri  kwa mujibu wa mamlaka aliyopewa na Kifungu Namba 17 cha sheria ya magonjwa ya Mifugo Namba 17 ya mwaka 2003 ametangaza rasmi kwamba Wilaya ya Dodoma Mjini inamlipuko wa ugonjwa wa Homa ya nguruwe na kwa sasa ameweka zuio la biashara ya Nguruwe na mazao yake hadi hapo itakapotangazwa vinginevyo. 
Katika kipindi cha zuio: 
  • Hakuna mnyama yeyote jamii ya nguruwe (Ngiri, nguruwe pori au nguruwe wa kufugwa) ataruhusiwa kuingia, au kutoka nje ya eneo la Wilaya ya Dodoma pasipokuwa na ruhusa ya maaandishi kutoka kwa Daktari wa Mifugo wa Wilaya ya Dodoma.
  • Pia hakuna bidhaa inayotokana na nguruwe, ikiwemo mbolea, kinyesi, mkojo na damu kitakacho ruhusiwa kuingia au kutoka nje ya Wilaya ya Dodoma pasipokuwa na ruhusa ya maandishi kutoka kwa Daktari wa Mifugo wa Wilaya ya Dodoma Mjini.
  • Aidha, hakuna mnyama yeyote wa jamii iliyotajwa hapo juu atakayekusanywa kwa ajili ya biashara pasipokuwa na ruhusa ya maandishi kutoka kwa Daktari wa Mifugo wa Wilaya ya Dodoma. 
  • Uchinjaji wa nguruwe ndani ya Wilaya ya Dodoma, utafanyika chini ya usimamizi madhubuti wa mtaalam wa afya za mifugo mwenye dhamana.

No comments:

Post a Comment