Monday, June 5, 2017

OFISI YA MAKAMU WA RAIS YAPONGEZA JUHUDI ZA KUTUNZA MAZINGIRA MANISPAA YA DODOMA


Ofisa Mazingira wa Idara ya Mazingira katika Ofisi ya Makamu wa Rais Timotheo Mande alipokuwa akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika kwa ngazi ya Wilaya katika viwanja vya ‘Nyerere Square’ Manispaa ya Dodoma.


Wawakilishi wa vikundi mbalimbali vya usafi na utunzaji wa Mazingira ktika Manispaa ya Dodoma wakiwa na vifaa vyao walivyokabidhiwa na Manispaa hiyo ili kuimarisha shughuli za Usafi na Utunzaji wa  Mazingira katika Manispaa hiyo. Vifaa vyenye thamani ya shilingi milioni 4 vilitolewa. PICHA ZOTE NA RAMADHANI JUAM-OFISI YA MKURUGENZI




OFISI ya Makamu wa Rais imepongeza jitihada zinazofanywa na Manispaa ya Dodoma katika kuuweka mji wa Dodoma katika hali ya usafi ikiwemo kuimarisha vikundi vya usafi kwa kuwapatia vifaa mbalimbali vya kufanyia usafi.

Pongezi hizo zilitolewa jana na Ofisa Mazingira wa Idara ya Mazingira katika Ofisi ya Makamu wa Rais Timotheo Mande alipokuwa akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika kwa ngazi ya Wilaya katika viwanja vya ‘Nyerere Square’ Manispaa ya Dodoma.

Alielezea kufurahishwa na namna Manispaa inavyoshirikiana na kuvisaidia vikundi vya usafi na utunzaji wa Mazingira ambapo katika maadhimisho hayo alishuhudia vikundi nane vikikabidhiwa vifaa mbalimbali vya usafi vyenye thamani ya shilingi milioni 4.

No comments:

Post a Comment