Thursday, June 8, 2017

MKUU WA WILAYA YA DODOMA CHRISTINE MNDEME KUVILEA VIKUNDI VYA USAFISHAJI NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA MANISPAA YA DODOMA


MKUU wa wilaya ya Dodoma Mheshimiwa Christine Mndeme akihutubia wadau wa Mazingira (hawapo pichani) katika sherehe za maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani Juni 5 mwaka huu katika viwanja vya Nyerere Square Mjini Dodoma .
MKUU wa wilaya ya Dodoma Mheshimiwa Christine Mndeme akikagua mabanda ya wadau wa utunzaji wa Mazingira kwa njia ya ufugaji nyuki. 
MKUU wa wilaya ya Dodoma Mheshimiwa Christine Mndeme akikagua mabanda ya wadau wa utunzaji wa Mazingira kwa njia ya kuchoma mkaa bila kukata miti badala yake wanatumia pumba. 
MKUU wa wilaya ya Dodoma Mheshimiwa Christine Mndeme akikabidhi vifaa vya usafishaji wa mazingira kwa viongozi wa vikundi vya usafishaji wa Mazingira Manispaa ya Dodoma 
MKUU wa wilaya ya Dodoma Mheshimiwa Christine Mndeme akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanavikundi vya usafishaji na utunzaji wa Mazingira Manispaa ya Dodoma. PICHA ZOTE NA RAMADHANI JUMA-OFISI YA MKURUGENZI

MKUU wa wilaya ya Dodoma Mheshimiwa Christine Mndeme amekubali jukumu la kuwa mlezi wa vikundi mbalimbali vya usafi na utunzaji wa Mazingira vilivyopo katika Manispaa ya Dodoma, hatua ambayo pia itamuweka karibu zaidi na vikundi hivyo  katika kazi muhimu ya kuuweka mji  huo katika hali ya usafi na kuvutia ikizingatiwa kuwa ndio Makao Makuu ya Nchi na tayari Serikali imeshahamia mjini humo.

Mheshimiwa  Mndeme alitangaza hatua hiyo wakati wa maadhimisho ya kilele cha Siku ya Mazingira Duniani Juni 5 mwaka huu kwa ngazi ya Wilaya yaliyofanyika katika viunga vya Bustani ya Nyerere Square mjini Dodoma.

Katika sherehe hizo, Mkuu huyo wa Wilaya pia alikagua mabanda ya wadau wa utunzaji wa Mazingira na  kugawa  vifaa mbalimbali vya kufanyia usafi  kwa vikundi nane vya usafi  vyenye thamani ya shilingi milioni 4.


Sherehe hizo zilihudhuriwa pia na Naibu Meya wa Manispaa ya Dodoma Jumanne Ngede, Ofisa Mazingira wa Manispaa hiyo Dickson Kimari amabaye alimuwakilisha pia Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi, Ofisa Mazingira kutoka Idara ya Mazingira katika Ofisi ya Makamu wa Rais Timotheo Mande pamoja na wadau wengine. 

No comments:

Post a Comment