Thursday, December 21, 2017

MAKAMU WA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AZINDUA DODOMA YA KIJANI, AAGIZA HALMASHAURI ZA MKOA HUO KUTUNGA SHERIA NDOGO ZITAKAZOMTAKA KILA MKAZI KUPANDA MITI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiandaa mti wake kabla ya kuupanda mara baada ya kuzindua  programu ya upandaji miti ili kuufanya mji wa Dodoma kuwa wa Kijani iliyofanyika kwenye chanzo cha maji cha Mzakwe Kata ya Makutupora Mjini Dodoma jana. PICHA ZOTE: RAMADHAI JUMA-OFISI YA MKURUGENZI MANISPAA YA DODOMA
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipanda mti wake mara baada ya kuzindua  programu ya upandaji miti ili kuufanya mji wa Dodoma kuwa wa Kijani iliyofanyika kwenye chanzo cha maji cha Mzakwe Kata ya Makutupora Mjini Dodoma jana. PICHA ZOTE: RAMADHAI JUMA-OFISI YA MKURUGENZI MANISPAA YA DODOMA
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dokta Binilith Mahenge akipanda mti katika eneo la Mzakwe Kata ya Makutupora Manispaa ya Dodoma huku akisaidiwa na Kocha Mkuu wa Timu ya Soka ya Dodoma FC Jamhuri Kihwelu 'Julio' (mwenye kofia ya kijani) mara baada ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan kuzindua programu ya  upandaji miti na kuufanya Mkoa wa Dodoma kuwa wa Kijani.
Meya wa Manispaa ya Dodoma Mstahiki Profesa Davis Mwamfupe akinyeshea mti  alioupanda katika eneo la Mzakwe Kata ya Makutupora Manispaa ya Dodoma mara baada ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan kuzindua programu ya  upandaji miti na kuufanya Mkoa wa Dodoma kuwa wa Kijani.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi ( kulia ) akizungumza katika mahojiano ya moja kwa moja na mtangazaji wa kituo cha Televisheni cha Cluods Hassan Ngoma wakati wa uzinduzi wa programu ya upandaji miti uliofanywa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan  katika eneo la Mzakwe Kata ya Makutupora Manispaa ya Dodoma. 
Wananchi mbalimbali wakiendelea na zoezi la upandaji miti mara baada ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan kuzindua programu ya  upandaji miti na kuufanya Mkoa wa Dodoma kuwa wa Kijani, katika eneo la Mzakwe Kata ya Makutupora Manispaa ya Dodoma.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiazungumza kabla ya uzinduzi  wa programu ya upadaji miti ili kuufanya mji wa Dodoma kuwa wa Kijani iliyofanyika kwenye chanzo cha maji cha Mzakwe Kata ya Makutupora Mjini Dodoma jana. PICHA ZOTE: RAMADHAI JUMA-OFISI YA MKURUGENZI MANISPAA YA DODOMA


......................................................................

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amezitaka Halmashauri za Mkoa wa Dodoma kutunga Sheria Ndogo zitakazomtaka kila Mkazi wa eneo katika Mkoa huo kupanda miti ili kupambana na mabadiliko ya hali tabia Nchi.

Makamu wa Rais ametoa agizo hilo kwenye uzinduzi wa kampeni ya kuufanya mji wa Dodoma kuwa wa kijani iliyofanyika Desemba 21 mwaka huu katika eneo la Mzakwe Kata ya Makutupora Manispaa ya Dodoma.

Alisema upandaji miti si kwa ajili ya kuhifadhi mazingira tu bali ni fursa ya kiuchumi, kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi  ambapo alitolea mfano mti mmoja uliokomaa unaweza kunyonya kiasi cha kilogramu 150 za gesi ya hewa ya ukaa kwa mwaka na hivyo kusaidia kupunguza joto kwenye uso wa dunia, na pia kusaidia kuboresha afya ya mwili na akili.

“Ni dhahiri, kampeni hii ya kuifanya mji wa Dodoma kuwa wa kijani ni kuunga mkono uamuzi wa Rais wetu, Dkt. John Pombe Magufuli wa kuhamishia Makamo Makuu ya Nchi kutoka Dar es Salaam kuja Dodoma kwa vitendo.” Alisema.

Akihojiwa na Vyombo vya Habari wakati wa zoezi hilo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi alisema Manispaa ya Dodoma imejipanga kuugeuza Mji wa Dodoma kuwa kivutio kikubwa kimazingira kwani pamoja na kuhakikisha inasimamia na kutekeleza kwa ukamilifu program iliyozinduliwa na Makamu wa Rais, pia Manispaa itatenga eneo maalum la ukanda wa kijani (Green Belt) ili kuufanya Mji huo kuwa wa kipekee nchini.



No comments:

Post a Comment