Wednesday, December 20, 2017

RC ATEMBELEA DAMPO LA KISASA MANISPAA YA DODOMA, ASEMA DODOMA LAZIMA IWE SAFI ZAIDI


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dokta Binilith Mahenge (katikati mbele) akiwa na Mhandishi wa Mazingira wa Manispaa ya Dodoma Barnabas Faida (kulia) na Meneja wa Dampo la Kisasa la Manispaa hiyo John Chiwanga (kushoto) wakati Mkuu huyo wa Mkoa alipofanya ziara fupi katika Dampo hilo hivi karibuni.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dokta Binilith Mahenge (kushoto) akipokea taarifa fupi kuhusu Dampo la kisasa la Chidaya Manispaa ya Dodoma kutoka kwa Mhandishi wa Mazingira wa Manispaa hiyo Barnabas Faida (kulia) wakati Mkuu huyo wa Mkoa alipofanya ziara fupi katika Dampo hilo hivi karibuni.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dokta Binilith Mahenge (wa pili kushoto) akipatiwa maelezo kuhusu mfumo wa upimaji uzito wa taka zinazoletwa katika Dampo la kisasa la Chidaya Manispaa ya Dodoma unavyofanya kazi kutoka kwa Mhandishi wa Mazingira wa Manispaa hiyo Barnabas Faida (wa pili kulia) wakati Mkuu huyo wa Mkoa alipofanya ziara fupi katika Dampo hilo hivi karibuni. PICHA ZOTE: RAMADHANI JUMA-OFISI YA MKURUGENZI WA MANISPAA
Moja ya magari maalum kwa ajili ya kubeba uchafu ya Manispaa ya Dodoma likipimwa uzito kabla ya kuingia kumwaga uchafu katika Dampo hili la kisasa lilipo eneo la Chidaya Kata ya Matumbulu katika Manispaa hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dokta Binilith Mahenge (kushoto) akiwa katika sehemu ya Dampo la kisasa la Chidaya Manispaa ya Dodoma iliyoanza kutumika huku akipata maelezo kutoka kwa Mhandishi wa Mazingira wa Manispaa hiyo Barnabas Faida (kulia) wakati Mkuu huyo wa Mkoa alipofanya ziara fupi katika Dampo hilo hivi karibuni.
Sehemu ya pili ya Dampo la kisasa la Chidaya  katika Manispaa ya Dodoma linalotumia Teknolojia ya kuzika taka ardhini ambayo bado haijaanza kutumika kwa sasa.

 .........................................................

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Dokta Binilith Mahenge amesema Mji wa Dodoma hauna sababu ya kuwa mchafu kwa sababu Manispaa ya Dodoma imetekeleza mradi wa ujenzi wa dampo la kisasa na litakalodumu kwa miaka mingi ijayo.
 Aliyasema hayo baada ya kutembelea dampo la kisasa la Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma lililopo eneo la Chidaya Kata ya Matumbulu takribani umbali wa kilometa 12 kutoka katikati ya Mji wa Dodoma.

Katika ziara hiyo fupi, Mkuu huyo wa Mkoa alioongozana na Katibu Tawala wa Mkoa huo Rehema Madenge pamoja na Mkuu wa Idara ya Mazingira na Usafishaji wa Manispaa hiyo Dickson Kimaro aliyemwakilisha Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi.

Awali mara baada ya kuwasili katika eneo la dampo, Mheshimiwa Mahenge alielezwa jinsi Dampo hilo la kisasa linavyofanya kazi na Mhandisi wa Mazingira wa Manispaa ya Dodoma Barnabas Faida, aliyemweleza Mkuu wa Mkoa kuwa, dampo hilo linatumia teknolojia ya kuzika taka ardhini (Sanitary Landfill) ambayo ni rafiki kwa mazingira na afya za wakazi wa maeneo ya karibu na dampo.


Mhandisi Faida alimjulisha Mheshimiwa Mahenge kuwa, dampo hilo tayari limeanza kufanya kazi mapema mwaka huu, na limejengwa kwa fedha za mradi wa Kuimarisha Miji ya Kimkakati Tanzania (TSCP) unaofadhiliwa na Benki ya Dunia na kuratibiwa na Ofisi ya Rais-TAMISEMI.

No comments:

Post a Comment