Monday, April 23, 2018

KAZI YA UUZAJI WA VIWANJA 10,864 YAZIDI KUSHIKA KASI


Wateja wakieleweshwa eneo vilipo viwanja
Wateja wakiwa katika eneo maalum la kupumzikia wakati wakiendelea na taratibu za ununuzi wa viwanja

Mkuu wa Idara ya Ardhi Mipango Miji na Maliasili Joseph Mafuru (katikati) akishughulikia changamoto ya mteja.

..........................................
KAZI ya uuzaji wa Viwanja 10,684 imeendelea leo Jumatatu Aprili 23, 2018 katika eneo la Ofisi Kuu ya zamani ya Manispaa zilizopo jirani na Sabasaba.

Zoezi hilo lilianza siku ya Ijumaa Aprili 20, 2018, ambapo jumla ya wateja 399 walipatiwa Viwanja kwa ajili ya matumizi mbalimbali.

Katika awamu ya kwanza leo, wateja wapatao 400 wanaotarajiwa kuhudumiwa wamepatiwa kuponi za namba ikiwa ni sehemu ya utaratibu wa kuhudumiwa.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Idara ya Ardhi Mipango Miji na Maliasili Joseph Mafuru, zoezi la uuzaji wa Viwanja litaendelea mpaka Viwanja vyote vitakapomalizika na kwamba Wananchi wote wanakaribishwa.

No comments:

Post a Comment