Saturday, April 28, 2018

MADIWANI MWANZA WAWEKA HISTORIA JIJINI DODOMA

Diwani wa Kata ya Nyamagana Jijini Mwanza ambaye pia ni Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji hilo Mhe. Bhiku Kotecha (wa pili kushoto-mbele) akiwa na baadhi ya Madiwani na Wataalam wa Halmashauri hiyo walipotembelea Dampo la kisasa la kuhifadhia takataka lililopo eneo la Chidaya Jijini Dodoma jana. Mbele kushoto ni Mhandisi wa Mazingira wa Jiji la Dodoma Barnabas Faida na kulia ni Afisa Habari wa Jiji la Mwanza Martin Sawema. PICHA:DCC
Mhandisi wa Mazingira wa Jiji la Dodoma Barnabas Faida na (kuhoto) akitoa maelezo kuhusu mradi wa Dampo la kisasa la Chidaya kwa Madiwani na Wataalam wa Jiji la Mwanza waliotembelea eneo hilo jana Aprili 27, 2018 kwa lengo la kujifunza. 


Operesheni za kuhifadhi takataka zikiendelea katika Dampo la kisasa la Chidaya Jijini Dodoma.
Mhandisi wa Mazingira wa Jiji la Dodoma Barnabas Faida na (kuhoto) akifuatilia  maswali kuhusu mradi wa Dampo la kisasa la Chidaya kutoka kwa Madiwani na Wataalam wa Jiji la Mwanza waliotembelea eneo hilo jana Aprili 27, 2018 kwa lengo la kujifunza. 
Muonekano wa sehemu ya Dampo la kisasa la Chidaya Jijini Dodoma ambayo bado haijaanza kutumika.


................................................................
MADIWANI wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza wameingia kwenye historia ya kuwa wageni wa kwanza kufanya ziara ya kubadilishana uzoefu katika Halmashauri ya Jiji jipya la Dodoma mara baada ya iliyokuwa Manispaa ya Dodoma kupandishwa hadhi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Magufuli wakati wa Sherehe za miaka 54 ya Muungano Aprili 26, mwaka huu zilizofanyika katika uwanja ya Jamhuri Jijini humo.

Madiwani hao wa jiji la Mwanza wakiongozwa na Naibu Meya Mhe. Bhiku Kotecha ambaye ni Diwani wa Kata ya Nyamagana, walitembelea Halmashauri ya Jiji la Dodoma jana Aprili 27, 2018 ikiwa ni siku moja tangu iliyokuwa Manispaa ya Dodoma kupewa hadhi ya Jiji.

Lengo la ziara hiyo ilikuwa ni kubadilishana uzoefu hususan katika suala la Usafi wa Mazingira, ambapo walitembelea Dampo la kisasa la kuhifadhia takataka kwa njia ya kuzifukia (Sanitary Land Fill) lililopo eneo la Chidaya Kata ya Matumbulu nje kidogo ya Jiji la Dodoma.

Wakiwa katika eneo la Dampo, walipata maelezo ya kina juu ya mradi huo kutoka kwa Mhandisi wa Mazingira wa Jiji la Dodoma Barnabas Faida, ambaye aliwaeleza kuwa, mradi huo umetekelezwa kwa awamu kuanzia mwaka 2011 kwa Fedha za Serikali Kuu ikiwa ni mkopo wa Benki ya Duniani kupitia mradi wa kuimarisha Majiji ya Kimkakati (TSCP) na kwamba hadi kukamilika kwake umegharimu zaidi ya Shilingi Bilioni 7.1, huku ukiwa tayari umeanza kufanya kazi.


No comments:

Post a Comment