Monday, April 16, 2018

ZAIDI YA VIWANJA ELFU KUMI VYAINGIA SOKONI DODOMA




...............................................................
HALMASHAURI ya Manispaa ya Dodoma inatarajia kuuza Viwanja 10,864 kwa ajili ya matumizi mbalimbali ikiwemo Makazi, Biashara, Makazi na Biashara, Taasisi na Viwanda.
 Akiongea na Waandishi wa Habari Mjini Dodoma mwishoni mwa wiki, Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Godwin Kunambi amesema kuwa, Viwanja hivyo vipo katika maeneo ya  Mtumba na Iyumbu kando ya barabara kuu ya Dodoma - Dar es Salaam.
Amesema Viwanja hivyo vitaanza kuuzwa siku ya Ijumaa Aprili 20, 2018 kuanzia saa 2:00 asubuhi katika eneo la Ofisi za Manispaa (Ofisi kuu ya zamani ya Manispaa) zilizopo jirani na Sabasaba.

KWA TAARIFA YA KINA SOMA HAPA CHINI;
Bei za Viwanja zitakuwa kama ifuatavyo kwa mita moja ya mraba:
ENEO LA MTUMBA
UKANDA WA BARABARA YA LAMI
  • Makazi                          8,000/=
  • Makazi na Biashara      8,500/=
  • Biashara                     10,000/=
  • Taasisi                          7,000/=
  • Viwanda vidogo          20,000/=
UKANDA WA KATI
  • Makazi                          6,000/=
  • Makazi na Biashara      7,500/=
  • Biashara                       8,000/=
  • Taasisi                          5,000/=
  • Viwanda vidogo          15,000/=
UKANDA WA BARABARA YA KIKOMBO
  • Makazi                         3,000/=
  • Makazi na Biashara     5,500/=
  • Biashara                      6,000/=
  • Taasisi                         5,000/=
  • Viwanda vidogo         10,000/=
ENEO LA IYUMBU
  • Makazi                         6,000/=
  • Makazi na Biashara     8,000/=
  • Biashara                    15,000/=
  • Taasisi                         7,000/=
  • Viwanda vidogo         20,000/=
Mauzo ya Viwanja yatafanyika kuanzia Ijumaa ya tarehe 20/04/2018. Utaratibu wa mauzo utakuwa kama ifuatavyo:
Kwa wananchi walioomba viwanja Manispaa watafika kwenye eneo la ofisi za zamani za Halmashauri na kuhakiki majina yao ambayo yatakuwa yamebandikwa kwenye mbao za matangazo. Ni lazima mwananchi afike na kitambulisho cha kumtambulisha. Kabla ya kuchagua kiwanja mwananchi anatakiwa kulipa Tshs. 20,000/= za fomu.
Mwananchi akishachagua kiwanja atapewa hati ya madai ya kiwanja hicho na kutakiwa kulipa fedha zote ndani ya siku Thelathini (30) tangu tarehe aliyopokea hati ya madai.
Kwa watumishi wa Umma wanaohamia Dodoma watapelekewa hati ya madai kupitia Makatibu Wakuu wa Wizara zao na watatakiwa kufanya malipo ndani ya siku Thelathini (30).

No comments:

Post a Comment