![]() |
Washiriki wakiwa wameketi kando ya vikombe vilivyotolewa kwa washindi |
..................................................
HALMASHAURI
ya Jiji la Dodoma imeibuka mshindi wa jumla baada ya kushinda michezo mingi katika michezo ya Shule za
Sekondari (UMISETA) iliyofanyika kwa siku tatu kuanzi Mei 26, 2018 na kushirikisha
zaidi ya Wanamichezo 700 kutoka katika Wilaya zote za Mkoa wa Dodoma, huku
Wilaya ya Kongwa ikishika nafasi ya pili na Mpwapwa nafasi ya tatu.
Timu
ya Wanamichezo wa Jiji la Dodoma iliibuka bingwa wa Mkoa baada ya kushinda
michezo ya Mpira wa Mikoni kwa Wavulana, Mpira wa Pete, Mpira wa Miguu kwa
Wasichana, Kikapu kwa Wavulana na Wasichana, kurusha tufe, kurusha kisahani,
Mkuu
wa Idara ya Elimu Sekondari wa Jiji la Dodoma Mwalimu Abdallah Membe amesema
amefurahishwa na ushindi walioupata na kwamba wao kama Jiji walijipanga vizuri,
huku akiwapongeza wote waliofanikisha mafanikio hayo wakiwemo Wanafunzi,
Walimu, na wadau wengine wote.
Amesema
baada ya hatua hiyo kufikia tamati, timu ya Mkoa ya Michezo hiyo itasafiri
Jumapili wiki hii kuelekea Jijini Mwanza kushiriki michezo hiyo kwa ngazi ya
Taifa inayotarajiwa kuanza Jumatatu Mei 4 mwaka huu Jijini humo.
No comments:
Post a Comment