Wednesday, May 30, 2018

JIJI LA DODOMA VINARA UMISETA


Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari wa Jiji la Dodoma Mwalimu Abdallah Membe akionesha kikombe cha ubingwa wa Michezo ya UMISETA Kimkoa iliyofanyika kwa siku tatu katika Viwanja vya Sekondari ya Dodoma kuanzia Mei 26 mwaka huu. 
Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari wa Jiji la Dodoma Mwalimu Abdallah Membe akipokea kikombe cha ubingwa wa Michezo ya UMISETA Kimkoa iliyofanyika kwa siku tatu katika Viwanja vya Sekondari ya Dodoma kuanzia Mei 26 mwaka huu. 
Washiriki wakiwa wameketi kando ya vikombe vilivyotolewa kwa washindi


..................................................

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imeibuka mshindi wa jumla baada ya kushinda michezo mingi katika michezo ya Shule za Sekondari (UMISETA) iliyofanyika kwa siku tatu kuanzi Mei 26, 2018 na kushirikisha zaidi ya Wanamichezo 700 kutoka katika Wilaya zote za Mkoa wa Dodoma, huku Wilaya ya Kongwa ikishika nafasi ya pili na Mpwapwa nafasi ya tatu.

Timu ya Wanamichezo wa Jiji la Dodoma iliibuka bingwa wa Mkoa baada ya kushinda michezo ya Mpira wa Mikoni kwa Wavulana, Mpira wa Pete, Mpira wa Miguu kwa Wasichana, Kikapu kwa Wavulana na Wasichana, kurusha tufe, kurusha kisahani,
na riadha kwa mita 200.

Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari wa Jiji la Dodoma Mwalimu Abdallah Membe amesema amefurahishwa na ushindi walioupata na kwamba wao kama Jiji walijipanga vizuri, huku akiwapongeza wote waliofanikisha mafanikio hayo wakiwemo Wanafunzi, Walimu, na wadau wengine wote.

Amesema baada ya hatua hiyo kufikia tamati, timu ya Mkoa ya Michezo hiyo itasafiri Jumapili wiki hii kuelekea Jijini Mwanza kushiriki michezo hiyo kwa ngazi ya Taifa inayotarajiwa kuanza Jumatatu Mei 4 mwaka huu Jijini humo.


No comments:

Post a Comment