Friday, May 18, 2018

WAZIRI LUGOLA AANZA ZIARA YA WIKI MANISPAA YA DODOMA


Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Kangi Lugola (wa pili kulia) akikagua mifumo ya usimamizi wa Mazingira katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma jana. Kushoto ni Afisa Mazingira wa Manispaa ya Dodoma Dickson Kimaro na pili kushoto ni Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mzee Nassoro. Wa tatu kutoka kulia ni Afisa Afya wa Mkoa wa Dodoma Carle Lyimo. PICHA ZOTE-RAMADHANI JUMA
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mzee Nassoro akitoa maelezo kwa Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Kangi Lugola (katikati) wakati wa ziara ya kiongozi huyo katika hosptali hiyo jana.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Kangi Lugola (kulia) akikagua mifumo ya usimamizi wa Mazingira katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma jana. Kulia ni Afisa Afya wa Mkoa wa Dodoma Carle Lyimo.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Kangi Lugola akiwa katika sehemu ya Vyoo ya moja ya Wodi ya wagonjwa  akikagua mifumo ya usimamizi wa Mazingira katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma jana.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Kangi Lugola (kulia) akihakiki moja ya 'chemba' za mifumo ya maji katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu John wakati alipofanya ziara ya kukagua mifumo ya usimamizi wa Mazingira chuoni hapo jana.



..........................................................................


NAIBU Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Kangi Lugola ameanza ziara ya kikazi ya wiki moja katika Manispaa ya Dodoma jana ambapo alitembelea Ofisi za Halmashauri na kupokea taarifa ya hali ya Mazingira kwa ujumla iliyowasilishwa na Mkuu wa Idara ya Mazingira na udhibiti wa taka ngumu Dickson Kimaro.

Naibu Waziri pia alipata taarifa kutoka kwa wataalam wa taasisi zingine ambazo ni wadau wa Mazingira ikiwemo Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA), Idara ya Madini, na Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) ambao amefutana nao katika ziara hiyo.

Katika siku ya kwanza ya ziara yake hapo jana, Naibu Waziri Lugola alitembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma na Chuo Kikuu cha Mtakatifu John ambapo alikagua mifumo ya usimamizi wa taka ambapo kwa ujumla alikiri kuridhishwa jinsi taasisi hizo zinavyozingatia matakwa ya Sheria na taratibu za kuhifadhi Mazingira, lakini aliziagiza kuhakikisha takataka zinazoteketezwa kwa kuchomwa moto zinateketea kwa kiwango kinachokubalika.


Ziara ya Naibu Waziri inaendelea leo Ijumaa Mei 18, 2018 ambapo pamoja na maeneo mengine, atatembelea na kukagua mifumo ya usimamizi wa taka katika machinjio ya Punda iliyopo eneo la Kizota   na inatarajiwa kumalizika Mei 25, mwaka huu.     



No comments:

Post a Comment