Thursday, July 28, 2016

MICHUZI BLOG: Manispaa ya Dodoma yafanikiwa kukusanya asilimia 80.28 ya mapato

MANISPAA YA DODOMA YAFANYA VIZURI KWENYE MAKUSANYO YA KODI

HALMASHAURI ya Manispaa ya Dodoma imefanikiwa kukusanya asilimia 80.28 ya mapato kutoka katika vyanzo vyake mbalimbali vya ndani katika mwaka wa fedha 2015/2016 uliomalizika Juni 30 mwaka huu.

Katika mwaka huo wa fedha Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma ilipanga kukusanya shilingi 4,566,075,181 kutoka katika vyanzo vyake vya ndani (own sources) ambapo mpaka mwisho wa mwaka huo makusanyo halisi ni 3,665,699,279 sawa na asilimia 80.28 ya makisio.

Akizungumza katika kikao cha mwaka cha Baraza la Halmashauri ya Manispaa hiyo, Meya wa Manispaa hiyo Mstahiki Jaffar Mwanyemba aliwaambia wajumbe wa Baraza hilo kuwa, mafanikio hayo yametokana na uchapaji kazi wa watendaji na madiwani wa Manispaa hiyo.

Mstahiki Mwanyemba aliwapongeza wote waliohusika kwa namna yeyote katika kufikia hatua hiyo huku akitoa wito kwa Ofisi ya Mkurugenzi na Madiwani wa kuimarishwa kwa juhudi zaidi katika ukusanyaji katika mwaka wa fedha 2016/2017.

"Mwaka mpya wa fedha umeshaanza hivyo Mkurugenzi na watendaji wako anzeni kukusanya kodi mapema...na waheshimiwa madiwani tuongeze nguvu katika kusimamia vyanzo vya mapato katika maeneo yetu" alisema.

Aidha, katika mkutano huo ambao kwa mujibu wa kanuni unakuwa na ajenda mbili tu ambazo ni kujadili taarifa ya utendaji na uwajibikaji wa Halmashauri kwa mwaka uliopita na kupitia na kupitisha ratiba ya vikao vya Halamshauri kwa mwaka unaofuata, wajumbe walipitisha ratiba ya vikao vya Halmashauri hiyo kwa mwaka wa fedha 2016/2017 .   

Tuesday, July 26, 2016

MAJALIWA AZUNGUMZA NA WANADODOMA KUHUSU MIKAKATI YA KUHAMIA MAKAO MAKUU.

MSTAHIKI MEYA DODOMA “TUENZI MASHUJAA KWA KUFANYAKAZI”

NA IMMACULATE MAKILIKA-MAELEZO, Dodoma
Mstahiki Meya wa mji wa Dodoma Jaffari Mwanyemba, amesema kuwa  watanzania wanatakiwa kuwaenzi Mashujaa waliopigana katika  vita mbalimbali  ikiwa ni katika harakati za kuiletea  uhuru  nchi ya Tanzania.
Hayo yamesemwa  leo saa sita usiku, wakati alipokuwa akizima Mwenge wa uhuru uliowashwa jana  Julai 24,  na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini  Mheshimiwa Christina Mndeme katika kilele cha mnara wa mashujaa mnano saa 6 kamili usiku ikiwa ni sehemu ya  maombolezo ya kumbukumbu ya Mashujaa, yaliyofanyika katika Uwanja wa Mashujaa uliopo mjini Dodoma.
“Watanzania tuna jukumu la kuwaenzi Mashujaa  kwa kufanyakazi kwa bidii, nidhamu na uadilifu, na kama wote tutafanya hivyo tutakuwa tumewaenzi mashujaa wetu” alisema Mstahiki Meya Mwanyemba
Ameongeza kuwa kila mwananchi atimize uwajibu wake kwa kufanyakazi, ili kila mmoja atapata haki yake na hivyo kuendelea kudumisha amani iliyopo nchini.
Maadhimisho ya kumbukumbu za Mashujaa kwa mwaka huu yamefanyika leo julai 25, mkoani Dodoma ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli alikuwa  mgeni rasmi katika maadhimisho hayo.

VIKUNDI VYA USHIRIKA NA WAJASIRIAMALI DODOMA WATAKIWA KUJITANUA KIMIRADI


VIKUNDI mbalimbali vya wanaushirika na wajasiriamali katika Manispaa ya Dodoma wameshauriwa kuweka mipango ya kuongeza miradi zaidi ili kukuza mitaji yao na kufikia malengo ya kuundwa kwa vikundi hivyo.

Ushauri huo umetolewa na Naibu Meya wa Manispaa ya Dodoma Jamanne Ngede wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi iliyofanywa na wajumbe wa Kamati ya Fedha na Utawala katika Kata mbalimbali za Manispaa hiyo.
Aliwataka wanaushirika na vikundi vingine vya wajasiriamali kuunda vikundi vidogo miongoni mwao na kupeana mitaji ili kukuza wigo wa kazi zao na hivyo kujiongezea kipato zaidi.
Miongoni mwa vikundi vilivyokaguliwa na Kamati hiyo ni kikundi cha Kasi Mpya kilichopo katika Kata ya Msalato ambacho ni cha akina mama wanaojishughulisha na ufugaji wa kuku wa mayai na utengenezaji wa batiki.
Kikundi hicho chenye wanachama kumi kina kuku 300 wa mayai ambapo kwa siku moja hukusanya kati ya trei sita hadi kumi za mayai, huku trei moja ya mayai ikiwa na thamani ya shilingi 8,500.
Katika kukiongezea nguvu kikundi hicho cha akina mama, Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma imekipatia mkopo wa shilingi 806,450 kwa ajili ya kununua chakula cha kuku na madawa ambapo tayari kimeanza kufanya marejesho ya mkopo huo kwa kutoa shilingi 148,000.

 Naibu Meya wa Manispaa ya Dodoma Jamanne Ngede (mwenye kaunda suti) na ujumbe wake wakitazama kuku waliopo katika moja ya mabanda ya wajasiriamali wa kikundi cha akina mama cha Kasi Mpya kilichopo katika Kata ya Msalato katika Manispaa hiyo. Akina mama hao wanafuga kuku wa mayai wapatao 300.


  Baadhi ya kuku wanaofugwa na akina mama hao

 Kati ya trei 6 hadi 10 za mayai huokotwa kwa siku


 Baadhi ya akina mama ambao ni wanachama wa kikundi hicho


 Naibu Meya wa Manispaa ya Dodoma Jamanne Ngede (kulia) akipokea zawadi ya mayai kwa niaba ya Kamati ya Fedha na Utawala kutoka kwa wajasiriamali hao.

 Naibu Meya wa Manispaa ya Dodoma Jamanne Ngede (kulia) akivishwa zawadi ya batiki aliyopewa na wajasiriamali wa kikundi cha akina mama cha Kasi Mpya kilichopo katika Kata ya Msalato katika Manispaa hiyo. 


Naibu Meya wa Manispaa ya Dodoma Jamanne Ngede (aliyejifunika batiki katikati waliokaa) na wajumbe wengine wa Kamati ya Fedha na Utawala wa Manispaa ya Dodoma John Matonya (kushoto) na Jamal Ngalya (wa pili kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na kikundi wajasiriamali cha akina mama cha Kasi Mpya kilichopo katika Kata ya Msalato katika Manispaa hiyo, na baadhi ya wataalam wa Manispaa hiyo. 

Wednesday, July 20, 2016

 MAJALIWA AWEKA JIWE LA MSINGI LA UPANUZI NA UKARABATI UWANJA WA NDEGE DODOMA

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA KUWEKA JIWE LA MSINGI UKARABATI WA UWANJA WA NDEGE WA DODOMA


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANI

                                                  WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO                                                     
MAMLAKA YA VIWANJA VYA NDEGE
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim M. Majaliwa kesho, tarehe 20/07/2016, anatarajiwa kuweka jiwe la msingi la mradi wa ukarabati na upanuzi wa Kiwanja cha ndege cha Dodoma.
Ukarabati huo utajumuisha urefushaji wa barabara ya kuruka na kutua ndege hadi kufikia urefu wa kilometa 2.5 kutoka Kilometa 2 za awali.
Kurefushwa kwa barabara hiyo, sasa kutatoa fursa kwa ndege kubwa Bombardier Q400, Gulfstream 550, ATR 72 n.k zenye uwezo wa kubeba abiria 90.
Ukarabati huo unafanyika kwa fedha za Serikali ya Tanzania na unasimamiwa na Wahandisi wa Mamlaka ya Viwanja Vya Ndege Nchini kwa ushirikiano  na Wakala wa Barabara nchini (TANROADS).
Ukarabati na upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Dodoma ni miongoni  mwa Miradi mbali mbali inayotekelezwa na Mamlaka ya viwanja Vya Ndege nchini kama vile Viwanja vya Tabora, Bukoba, Kigoma na Mwanza ambayo imekwisha anza na miradi mipya ya viwanja vya ndege vya Shinyanga na Sumbawanga itakayoanza hivi karibuni.
Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) ni wakala wa viwanja vya ndege iliyoanzishwa kwa Tangazo la Serikali Namba 404 la mwaka 1999, chini ya Sheria ya Wakala za Serikali Na. 30 ya mwaka 1997.
Dira:           Kuwa mtoaji wa Huduma za Viwanja vya Ndege kwa kiwango cha Kimataifa
                        Dhima:         Kutoa Huduma Bora na Viwezeshi katika Viwanja vya Ndege kwa kuzingatia ufanisi katika matumizi ya rasilimali zilizopo
Imani kuu za Mamlaka:
Kuwajali Wateja
Kuwaendeleza Wafanyakazi wa Mamlaka
Ulinzi na Usalama Viwanjani
Kufanya kazi kwa pamoja
Kuwa na Uongozi wa Mabadiliko
Uadilifu
IMETOLEWA NA KITENGO CHA SHERIA NA MAHUSIANO TAA
CHANZO: FULLSHANGWE BLOG

Monday, July 11, 2016

HALMASHAURI ZAPATA WAKURUGENZI WAPYA- Uteuzi wa Ra...

Halmashauri Zapata Wakurugenzi Wapya- Uteuzi wa Ra...: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli l...