Wednesday, March 29, 2017

MLYAMBATE Blog : WAKURUGENZI WA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA WACHAG...: Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya na Manispaa kote nchini kwa kauli moja wameridhia na kuwachagua viongozi watakaowawakilisha katika ku...
MLYAMBATE Blog : TOVUTI ZA SERIKALI HEWANI RASMI: TOVUTI ZA SERIKALI KUBORESHA USIMAMIZI NA USHIRIKISHWAJI WA WANANCHI Sekretarieti za mikoa yote 26 ya Tanzania Bara  na Halmashauri zake 18...

Wednesday, March 8, 2017

AUSTRIA KUWEKEZA DODOMA

Naibu Meya wa Jiji la Linz Austria Detlef Wimmer (aliyesimama) akitoa hotuba yake

Mtaalam wa ujenzi katika dampo la taka la kisasa lililopo Chidaya Manispaa ya Dodoma akitoa maelezo ya mradi kwa Naibu Meya wa jji la Linz la Austria Detlef Wimmer (wa pili kushoto). Kushoto ni Meya wa Manispaa ya Dodoma Mstahiki Jaffar Mwanyemba na wa  pili kulia ni Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Godwin Kunambi



Meya wa Manispaa ya Dodoma Mstahiki Jaffar Mwanyemba akizungumza na Wanahabari kuhusu ushirikiano wa Manispaa hiyo na jiji la Linz la Austria


Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi  akizungumza na Wanahabari kuhusu ushirikiano wa Manispaa hiyo na jiji la Linz la Austria


Ziara katika shamba la zabibu


Meya wa Manispaa ya Dodoma Mstahiki Jaffar Mwanyemba na Naibu Meya wa jiji la Linz la Austria Detlef Wimmer wakisaini hati ya makubaliano ya mashirikiano.

Meya wa Manispaa ya Dodoma Mstahiki Jaffar Mwanyemba na Naibu Meya wa jiji la Linz la Austria Detlef Wimmer wakionesha hati ya makubaliano ya mashirikiano mara baada ya kusaini.

Meya wa Manispaa ya Dodoma Mstahiki Jaffar Mwanyemba (wa pili kulia waliokaa) na Naibu Meya wa jiji la Linz la Austria Detlef Wimmer (wa pili kushoto waliokaa) wakiwa katika picha pamoja na baadhi ya watumishi manispaa hizo. Wa kwanza kulia waliokaa ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi na kwanza kushoto waliokaa  ni Kamishna Mkuu wa Jeshi la Zimamoto Tanzania Thobias Andengeye.  PICHA ZOTE NA RAMADHANI JUMA-OFISI YA MKURUGENZI, DMC






RAMADHANI JUMA
OFISI YA MKURUGENZI, DMC

Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma na jiji la Linz la nchini Austria zimesaini hati ya makubaliano (Memorandum of Understanding) ya ushirikiano katika nyanja za Utunzaji wa Mazingira, kuimarisha huduma za kijamii, uwekezaji wa kibiashara, kuimarisha miundombinu na teknolojia, na kuimarisha huduma ya kupambana na majanga ya moto na uokozi.

Maeneo mengine ambayo mamlaka hizo mbili zimekubaliana kushirikiana ni pamoja kutoa mafunzo mbalimbali wa watumishi wake na Madiwani wa pande zote mbili, kubadilishana watumishi pamoja na kushirikiana katika jambo lolote litakaloonekana kuwa na manufaa kwa wananchi wa pande zote.

Makubaliano hayo yalifikiwa hivi karibuni wakati wa  ziara ya siku moja ya  Naibu Meya wa jiji la Linz Detlef Wimmer na ujumbe wake katika Manispaa ya Dodoma ambapo alitembelea maeneo kadhaa ikiwemo Dampo la kisasa la takataka lililopo katika kijiji cha Chidaya kata ya Ntyuka Manispaa ya Dodoma na shamba la zabibu katika kata ya Mtumba ili kuangalia fursa za uwekezaji katika sekta ya kilimo.

Akisaini makubaliano hayo kwa niaba ya Manispaa ya Dodoma, Meya wa Manispaa hiyo Mstahiki Jaffar Mwanyemba alisema ushirikiano huo umekuja wakati muafaka na kwamba utakuwa na manufaa makubwa kwa wakazi wa miji hiyo huku akitoa wito kwa marafiki na wawekezaji wengine  kujitokeza kwani mji wa Dodoma kwa sasa umefunguka na kwamba ni wakati muafaka wa kuwekeza Dodoma.

 Kwa upande wake Naibu Meya wa jiji la Linz Detlef Wimmer ambaye alisaini hati hiyo kwa niaba ya mamlaka ya jiji hilo alielezea kuvutiwa kwake na mji wa Dodoma na kwamba amejifunza mengi katika ziara yake huku akiahidi ushirikiano wa dhati katika maeneo waliyokubaliana.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi alisema ushirikiano kati ya Manispaa ya Dodoma na Jiji la Linz ni mwanzo tu wa juhudi zinazofanywa na Manispaa katika kuweka mazingira rafiki  kwa wawekezaji mbalimbali ili kuhakikisha Manispaa hiyo inakua kwa kasi huku huduma za kijamii zikipewa kipaumbele kwa manufaa ya wakazi wake na hata wa mikoa ya  jirani.