Monday, June 25, 2018

MATIBABU YA KIBINGWA HOSPITALI TEMBEZI YAANZA LEO JUNI 25 JIJINI DODOMA





.................................................................
HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imeanza rasmi zoezi la siku 5 la kutoa huduma ya matatibu kwa wagonjwa mbalimbali kwa mfumo wa Hospitali Tembezi linalofanyika katika Hospitali Teule ya Wilaya Mtakatifu Gemma iliyopo Kata ya Miyuji Jijini humo.
Mganga Mkuu wa Jiji la Dodoma Hamad Nyembea amesema huduma ya Hospitali Tembezi ni jukwaa linalowakutanisha madaktari Bingwa wa fani mbalimbali za utabibu kama mgonjwa ya akina mama na watoto, Figo, Moyo, Koo na Pua, Kinywa na Meno, Shinikizo la Damu, Sukari, Tezi Dume, Shingo ya Kizazi, Macho, Masikio, pamoja na upasuaji wa mifupa na wa kawaida.
Ametoa wito kwa wakazi wa Jiji la Dodoma na Wilaya za jirani hususan wanaosumbuliwa na maradhi mbalimbali kutumia fursa hiyo vizuri.
"Kuna wagonjwa wengine ambao wameandikiwa rufaa kwenda Hospitali za mbali kama Muhimbili Dare es Salaam na hawana uwezo, hii ni fursa kwao kwani hapa kuna madaktari Bingwa wa fani zote na watahudumia kwa muda wa siku tano kuanzia leo, mpaka Ijumaa Juni 29.
Alifafanua kuwa utaratibu wa matibabu ni wa kawaida ambapo wagonjwa wenye Bima za Afya za NHIF na CHF watatibiwa kwa kutumia kadi zao na wale wasio na Bima watachangia Shilingi elfu 5 kama gharama ya kuonana na Daktari, na kwa huduma ya upasuaji mgonjwa atachangia Shilingi elfu 30 tu.

Thursday, June 21, 2018

JIJI ‘LAMWAGA’ MAMILIONI KWA VIJANA, WANAWAKE



Kaimu Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii wa Jiji la Dodoma Mufungo Manyama akizungumza na viongozi wa vikundi 137 vya Wanawake na Vijana wakati wa semina elekezi kwa viongozi hao kuhusu uendeshaji wa vikundi na matumizi ya fedha za mikopo kabla ya kupatiwa mkopo wa milioni 344 mapema wiki ijayo.

Kaimu Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii wa Jiji la Dodoma Mufungo Manyama akizungumza na viongozi wa vikundi 137 vya Wanawake na Vijana wakati wa semina elekezi kwa viongozi hao kuhusu uendeshaji wa vikundi na matumizi ya fedha za mikopo kabla ya kupatiwa mkopo wa milioni 344 mapema wiki ijayo.

Kaimu Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii wa Jiji la Dodoma Mufungo Manyama akizungumza na viongozi wa vikundi 137 vya Wanawake na Vijana wakati wa semina elekezi kwa viongozi hao kuhusu uendeshaji wa vikundi na matumizi ya fedha za mikopo kabla ya kupatiwa mkopo wa milioni 344 mapema wiki ijayo.

Kaimu Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii wa Jiji la Dodoma Mufungo Manyama akizungumza na viongozi wa vikundi 137 vya Wanawake na Vijana wakati wa semina elekezi kwa viongozi hao kuhusu uendeshaji wa vikundi na matumizi ya fedha za mikopo kabla ya kupatiwa mkopo wa milioni 344 mapema wiki ijayo.


.....................................................
HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma inatarajia kutoa takribani shilingi milioni 500 kwa ajili ya kukopesha vikundi vya Wajasiriamali Wanawake na Vijana kwa mwaka wa fedha unaomalizika Mwezi Juni, 2018.

Jumla ya vikundi 137 vinatarajiwa kunufaika na fedha hizo zinazotokana na makusanyo ya kodi za ndani ya Halmashauri (Own Source) ambapo  vikundi vya Wanawake ni 102 na vya vijana 37.

Akizungumza wakati akitoa semina elekezi kwa viongozi wa vikundi hivyo katika ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Dodoma leo Juni 21, 2018, Kaimu Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii wa Jiji la Dodoma Mufungo Manyama aliwaeleza wajumbe kuwa awamu ya mwisho ya mikopo kwa mwaka huu wa fedha itatolewa katikati ya wiki ijayo ambapo jumla ya Shilingi milioni 344 zitakabidhiwa kwa vikundi hivyo.

Aliwataka Wanavikundi hao kuwa makini na matumizi ya fedha wanazokopeshwa na kufanya marejesho kwa wakati ili wapate fursa ya kukopeshwa zaidi.

Kwa upande wao, baadhi ya viongozi wa vikundi hivyo waliishukuru Halmshauri ya Jiji na kuahidi kutumia mikopo hiyo kwa malengo yaliyokusudiwa ili waweze kurejesha kwa wakati hali itakayopelekea kunufaisha vikundi vingi zaidi.



Tuesday, June 5, 2018

WAKAZI DODOMA WAASWA KUKIJANISHA JIJI


Wadau mbalimbali katika Maandamano kuelekea Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma wakati wa kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani leo Juni 5, 2018.
Afisa Mazingira kutoka Idara ya Mazingira na Udhibiti wa Takangumu Jiji la Dodoma Ally Mfinanga akitoa neno la utangulizi kwa Mgeni rasmi katika maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani Naibu Meya wa Jiji hilo Jumanne Ngede (hayupo pichani) na wadau wengine katika Viwanja vya Nyerere Square leo Juni 5, 2018.

Mgeni Rasmi Naibu Meya Jumanne Ngede (wa pili kulia) akikagua mabanda ya wadau wa Mazingira

Mgeni Rasmi Naibu Meya Jumanne Ngede (wa pili kushoto) akikagua mabanda ya wadau wa Mazingira





....................................................................


NAIBU Meya wa Halmshauri ya Jiji la Dodoma Jumanne Ngede ametoa wito kwa kila mkazi wa Jiji hilo kuhakikisha anatunza Mazingira kwa kupanda miti katika maeneo yanayomzunguka ili kuunga mkono juhudu za Serikali na wadau kuhakikisha Jiji linakuwa la kijani kwa manufaa ya viumbe vyote.
Alitoa wito huo mapema leo asubuhi alipotembelea na kukagua mabanda ya wadau mbalimbali wa Mazingira walioshiriki kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere vilivyopo katikati ya Jiji la Dodoma leo Juni 5, 2018.   

Mhe. Ngede aliwapongeza wadu mbalimbali hususan wanaojihusisha na nishati mbadala kama Gesi na Sola ambazo matumizi yake yanasaidia kupunguza  ukataji wa miti na uharibufu wa misitu kwa ajili ya kuchoma mkaa unaotumika kwa kazi za jikoni.

Kwa upande wake, Afisa Mazingira kutoka Idara ya Mazingira na Udhibiti wa Takangumu Jiji la Dodoma Ally Mfinanga alisema Halmashauri imekuwa ikishikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha kila kundi katika jamii linawajibika katika kutunza Mazingira.

“Kuna wadau ambao tunashirikiana nao katika kutunza Mazingira kwa maana ya kupanda miti na kutunza misitu lakini pia, kama Halmashauri tunajukumu la kusafisha Mazingira kwa kuondosha taka zinazozalishwa Mjini…haya yote tunayatekeleza kwa kuwashirikisha pia wadau kama TFS na vikundi mbalimbali, vikiwemo vya kuzoa taka” alisema Mfinanga.

Kilele cha siku ya Mazingira Duniani huadhimishwa Juni 5 kila Mwaka na huambatana na jumbe mbalimbali kama sehemu ya kueleimisha Jamii, ambapo kaulimbiu ya Mwaka huu inasema “Mkaa ni gharama, tumia nishati mbadala”.