Thursday, May 25, 2017

MADIWANI MANISPAA YA DODOMA WAMPA KONGOLE RAIS MAGUFULI



Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Christina Mndeme (kulia) akiongoza wimbo maalum wa kumsifu na kumpongeza Mheshimiwa Rais wa Jamahuri ya Muungano wa Tanzania Dokta John Magufuli kwa uamuzi wake wa kuifuta Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) Katikati ni Naibu Meya  wa Manispaa Dodoma Jumanne Ngede na kushoto ni Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Godwin Kunambi


Waheshimiwa Madiwani ambao ni wajumbe wa Baraza la Madiwani la Manispaa ya Dodoma  wakiimba wimbo maalum wa kumsifu na kumpongeza Mheshimiwa Rais wa Jamahuri ya Muungano wa Tanzania Dokta John Magufuli kwa uamuzi wake wa kuifuta Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) Wimbo huo ulikuwa ukiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Christina Mndeme (Hayupo pichani).



BARAZA la Madiwani wa Manispaa ya Dodoma limempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dokta John Magufuli kwa hatua  yake ya kuivunja rasmi iliyokuwa Mamlaka ya Ustawishaji Makao  Dodoma (CDA) na kwamba hatua ni maamuzi muhimu na sahihi kwa maendeleo  ya Manispaa na Mkoa wa Dodoma kwa ujumla.

Wajumbe wa Baraza hilo likiongozwa na Mwenyekiti wake ambaye ni Naibu Meya  wa Manispaa hiyo Jumanne Ngede walikutana jana kwenye ukumbi wa Manispaa kwa ajili ya  Mkutano Maalum wa kuzungumza na vyombo vya Habari na kutoa  tamko rasmi la kumpongeza Rais Magufuli kwa hatua hiyo.

Walidai hatua hiyo itafungua milango kwa wawekezaji  wengi  kuwekea Dodoma kutokana  na taratibu za kupataji na umiliki wa ardhi kuboreshwa chini ya Manispaa, ikiwemo utolewaji wa hati za umiliki wa ardhi za miaka 99 badala zile za miaka 33 zilizokuwa zikitolewa na iliyokuwa CDA.


Mei 15 mwaka huu,  Mheshimiwa Rais Dokta John Magufuli alisaini tamko la Amri ya Rais la kuivunja iliyokuwa CDA baada ya kujiridhisha kuwa kwa sasa hakuna mahitaji ya kuwa na mamlaka hiyo iliyoanzishwa kwa Amri ya Rais mwaka 1973, na kwamba shughuli, mali, na watumishi 284 wanakuwa chini ya Manispaa ya Dodoma.

Wednesday, May 10, 2017

MALIASILI NA UTALII BLOG: BREAKING NEWS: TEMBO WANNE WAONEKANA CHUO KIKUU CH...: Tembo wakiwa wamejificha kwenye vichaka ndani ya eneo la Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) leo. Kwa mujibu wa taarifa za Wahifadhi wa Wanyama...

Friday, May 5, 2017

MADIWANI MANISPAA YA DODOMA WAMPONGEZA RAIS DOKTA MAGUFULI; WAPENDEKEZA CDA IVUNJWE


Katibu wa Mkutano wa Baraza la Madiwani wa Halmshauri ya Manispaa ya Dodoma ambaye pia ndiye Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Godwin Kunambi (kushoto) akiwasilisha taarifa ya Katibu mbele ya wajumbe wa Baraza hilo katika Mkutano wa kawaida wa robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2016/2017 jana katika ukumbi wa Manispaa. Kushoto kwake ni Naibu Meya wa Manispaa hiyo Jumanne Ngede   
Sehemu ya wajumbe wakifuatilia Mkutano wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma katika Ukumbi wa Manispaa hiyo jana.
Diwani wa Kata ya Mtumba Manispaa ya Dodoma Edward Maboje akichangia taarifa iliyowasilishwa na Katibu wa Baraza la Madiwani la Manispaa hiyo Godwin Kunambi iliyojumuisha agizo la Rais Dokta John Magufuli kuhusu uongozi wa Mkoa na wadau wote kuchunguza na kuishauri Serikali endapo kuna haja ya kuendelea au kutoendelea kuwa na Mamlaka ya Ustawishaji Makao (CDA). Madiwani kwa ujumla wao wamependekeza Mamlaka hiyo ivunjwe.
Baadhi ya Wataalam wa Manispaa ya Dodoma wakifuatilia Mkutano wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo katika Ukumbi wa Manispaa  jana. PICHA ZOTE: RAMADHANI JUMA

Na Ramadhani Juma
OFISI YA MKURUGENZI

MADIWANI wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma wameelezea kufurahishwa kwao na agizo alilotoa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dokta John Pombe Magufuli kuhusu kuundwa kwa timu itakayokuwa na kujumu la kufanya kuchunguza na kuishauri Serikali endapo kuna haja ya kuendelea kuwa na Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) katika kuendeleza mji wa Dodoma au jukumu hilo lifanywe na Halmashauri ya Manispaa kama ilivyo katika Manispaa zote nchini.

Wakichangia taarifa ya Katibu wa Baraza la Madiwani la Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi ambaye pia ndiye Mkurugenzi wa Manispaa hiyo jana, wajumbe wa Baraza hilo walidai kuwa sasa imefikia wakati Mamlaka hiyo uvunjwe kwani imekuwa ikisababisha migogoro mingi ya ardhi badala ya kuupanga Mji huo kwani ndio jukumu lao la msingi.

Madiwani wote waliopata fursa ya kuchangia taarifa hiyo walieleza kuwa, wananchi wa Manispaa ya Dodoma wamechoshwa na uwepo wa Mamlaka ya CDA na kwamba imewanyanyasa kwa muda mrefu ikiwa ni pamoja na kuwapora ardhi zao bila kuzingatia sheria na taratibu.



Hivi karibuni Mheshimiwa Rais Dokta John Magufuli akiwa Mjini Dodoma aliagiza pamoja na mambo mengine, kufanywa majadiliano kati ya wadau ambao ni uongozi wa Mkoa, Mamlaka ya Ustawishaji (CDA), Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma, Wizara ya Ardhi na mamlaka zote zinazohusika ili ziiishauri Serikali juu ya umuhimu wa kuendelea au kutoendelea na Mamlaka ya hiyo.