Tuesday, June 5, 2018

WAKAZI DODOMA WAASWA KUKIJANISHA JIJI


Wadau mbalimbali katika Maandamano kuelekea Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma wakati wa kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani leo Juni 5, 2018.
Afisa Mazingira kutoka Idara ya Mazingira na Udhibiti wa Takangumu Jiji la Dodoma Ally Mfinanga akitoa neno la utangulizi kwa Mgeni rasmi katika maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani Naibu Meya wa Jiji hilo Jumanne Ngede (hayupo pichani) na wadau wengine katika Viwanja vya Nyerere Square leo Juni 5, 2018.

Mgeni Rasmi Naibu Meya Jumanne Ngede (wa pili kulia) akikagua mabanda ya wadau wa Mazingira

Mgeni Rasmi Naibu Meya Jumanne Ngede (wa pili kushoto) akikagua mabanda ya wadau wa Mazingira





....................................................................


NAIBU Meya wa Halmshauri ya Jiji la Dodoma Jumanne Ngede ametoa wito kwa kila mkazi wa Jiji hilo kuhakikisha anatunza Mazingira kwa kupanda miti katika maeneo yanayomzunguka ili kuunga mkono juhudu za Serikali na wadau kuhakikisha Jiji linakuwa la kijani kwa manufaa ya viumbe vyote.
Alitoa wito huo mapema leo asubuhi alipotembelea na kukagua mabanda ya wadau mbalimbali wa Mazingira walioshiriki kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere vilivyopo katikati ya Jiji la Dodoma leo Juni 5, 2018.   

Mhe. Ngede aliwapongeza wadu mbalimbali hususan wanaojihusisha na nishati mbadala kama Gesi na Sola ambazo matumizi yake yanasaidia kupunguza  ukataji wa miti na uharibufu wa misitu kwa ajili ya kuchoma mkaa unaotumika kwa kazi za jikoni.

Kwa upande wake, Afisa Mazingira kutoka Idara ya Mazingira na Udhibiti wa Takangumu Jiji la Dodoma Ally Mfinanga alisema Halmashauri imekuwa ikishikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha kila kundi katika jamii linawajibika katika kutunza Mazingira.

“Kuna wadau ambao tunashirikiana nao katika kutunza Mazingira kwa maana ya kupanda miti na kutunza misitu lakini pia, kama Halmashauri tunajukumu la kusafisha Mazingira kwa kuondosha taka zinazozalishwa Mjini…haya yote tunayatekeleza kwa kuwashirikisha pia wadau kama TFS na vikundi mbalimbali, vikiwemo vya kuzoa taka” alisema Mfinanga.

Kilele cha siku ya Mazingira Duniani huadhimishwa Juni 5 kila Mwaka na huambatana na jumbe mbalimbali kama sehemu ya kueleimisha Jamii, ambapo kaulimbiu ya Mwaka huu inasema “Mkaa ni gharama, tumia nishati mbadala”.


No comments:

Post a Comment