Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi (kushoto) na Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Professa Dos Santos Silayo wakikabidhiana hati ya makubaliano. |
Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi (kushoto) akifafanua jambo mbele ya Mtendaji Mkuu ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Professa Dos Santos Silayo kuhusu maeneo waliyokubalina kupanda na kustawisha miti, na kuhifadhi misitu iliyopo ndani ya Jiji la Dodoma kwa lengo la kuikijanisha Dodoma.
........................................................................
HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma na Wakala ya
Huduma za Misitu Tanzania (TFS) zimesaini hati ya makubaliano (MOU) ya upandaji,
ustawishaji, na utunzaji wa miti na uhifadhi wa misitu iliyopo katika Jiji
hilo, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Kampeni ya Dodoma ya Kijani
iliyozinduliwa rasmi na Makamu wa Rais Mhe.
Samia Saluhu Hassan kwa kupanda miti kwenye eneo la Mzakwe mwishoni mwa mwaka
jana.
“Makubaliano haya yataliweka Jiji la Dodoma
katika ramani ya dunia katika kwenda na mahitaji ya maendeleo endelevu ya dunia
kupitia mpango uendelevu wa Miji, lazima tujipange kukabiliana na ongezeko la
watu na ukuaji wa Miji, Mpango huu utalifanya Jiji hili kwenda sambamba na kuweka
uwiano sawia wa kiikolojia.” Alisema Profesa Silayo.
Makubaliano hayo yamesainiwa ikiwa ni takribani
wiki mbili baada ya Jiji la Dodoma kuingia makubaliano na Mamlaka ya Hifadhi ya
Ngorongoro (NCA) ya utunzaji wa mizunguko mitatu mikubwa ya barabara iliyopo
Jijini humo, ambapo Mamlaka hiyo itahudumia bustani za maua na kuweka sanamu za
Wanyama ikiwemo ya Tembo ili kupendezesha Mji na kutangaza vivutio vya kitalii
vilivyopo Nchini.
No comments:
Post a Comment